KILIMO CHA MAHARAGWE MACHANGA/GREEN BEANS

maharagwe machanga yakiwa tayari yamevunwa


                       maharagwe machanga yakiwa bado shamba.

Hivi karibuni hapa nchini Tanzania, kumekuwa na uanzishaji na uendelezaji wa kilimo cha mazao mapya ambayo hayakuzoeleka hapo awali.   Moja ya mazao hayo ni pamoja na maharagwe machanga, maarufu kama Green beans au French beans.

Utayarishaji wa shamba

Lima shamba na kuondoa magugu yote. Hakikisha
kuwa umelima kwa kiwango ambacho udongo umelainika vya kutosha. Kabla ya kupanda ni lazima uhakikishe udongo umelainika vizuri na una maji ya kutosha siku mbili kabla ya kupanda. Hii inatege-meana na aina ya umwagiliaji, kwenye kilimo cha maharagwe machanga inapendekezwa zaidi kutumia umwa-giliaji wa matone.

Kupanda

Inashauriwa kuweka nafasi ya sentim-ita 30 kati ya mstari na mstari, na kati ya mmea na mmea sentimita 7. Panda mbegu moja kwa kila shimo.
Panda kwenye tuta na liwe na upana wa sen-timita 70, kati ya tuta na tuta kuwepo nafasi ya sentimita 80.     Ni vizuri kuacha nafasi ya sentimita 15 kutoka pembeni mwa tuta unapo-panda mbegu, ili kuepusha athari zin-azoweza kutokea na kuathiri mbegu au mmea baada ya kuota, mfano, mafu-riko. Endapo unatumia umwagiliaji wa mifereji inashauriwa kutengeneza makingo yenye kimo cha sentimita 15 na upana wa sentimita 70 kutoka kingo hadi kingo. Hii itasadia mimea kupata unyevu kwa urahisi pamoja na kinga ya magonjwa yanayosababishwa na unyevu uliopitiliza.


Kupanda

Inashauriwa kutumia mbolea ya kupandia zinazotokana na miamba kama vile DAP. Tumia gramu 5 kwa kila shimo. Hii itasaidia mizizi kuota kwa haraka. Usifukie mbegu kwa zaidi ya inchi 1.5.

Mbegu za maha-ragwe machanga huota baada ya siku Mbegu Inapendekezwa kutumia chotara aina ya F1. Aina hii ya mbegu imeonekana kuwa na mafani-kio makubwa zaidi ikiwa ni pamoja na uwezo wa kumudu magonjwa.       Inapendekezwa kupata mbegu kutoka kwa wazalishaji walioidhin-ishwa.Aina za mbegu na uwezo wake?

Boston

Aina hii ya mbegu ina uwezo mkubwa wa uzalishaji. Wakati wa mvua aina hii ya mbegu husham-buliwa zaidi na magonjwa hasa ya ukungu.?
Serengeti: Aina hii ina uzalishaji wa wastani. Aina hii ina uwezo mkubwa wa kuvumilia magonjwa.?

Tana:

 Aina hii uzalishaji wake ni mkubwa na wa muda mrefu. Inashambuliwa na magonjwa kwa wastani. Aina hii huhitaji kiwango kikubwa cha maji hasa wakati wa mavuno.Maharagwe machanga yamegawa-nyika katika makundi mawili;?
Maharagwe mateke kwa wastani (fine beans) na?Maharagwe mateke zaidi (extra fine beans)wataalamu walio karibu nawe.

  Epuka maharagwe kugusana na maji au tope wakati wa kuvuna kwani inaweza kusababisha ugonjwa wa kuvunda, hivyo kupata hasara. 
Baada ya kuvuna weka kwenye chombo chenye matundu kwa ajili ya kupitisha hewa. Hii ni wakati wa kuvuna kutoka shambani. Baada ya hapo, maharagwe yawekwe kwenye kreti maalumu na kuwekwa sehemu yenye ubaridi kusubiria uchambuzi na kuwekwa kwenye madaraja pamoja na kufungashwa. 

 
   Endapo mbegu hazikuota vizuri unaweza kurudishia si zaidi ya siku mbili tangu maharagwe yaote.UmwagiliajiHii inategemeana na hali ya hewa/msimu, kulingana na eneo ulipo. Kwa kawaida maharagwe haya hustawi kwenye udongo usiotuamisha maji, na iwe kwenye ukanda wenye baridi ya wastani.


Utunzaji

 Inapendekezwa kuwasiliana na mtaal-amu wa kilimo alie karibu nawe baada ya siku 14 ili kufanya ukaguzi sham-bani kuona kama kuna dalili zozote za wadudu pamoja na magonjwa kama vile mnyauko fuzari, endapo kuna dalili zozote shauriana na mtaalamu.   Mkulima anaweza kutumia mbolea kwa ajili ya kukuzia na kurutubisha majani kulingana na mahitaji.  
Ni lazima kupanda mahindi kuzun-guka shamba la maharagwe ili kuzuia upepo unaoweza kuharibu maharagwe yako na yasiwe na ubora unaotakiwa.

Palizi Ni muhimu kufanya palizi kuanzia baada ya siku kumi ili kuepusha makazi/maficho ya wadudu wahari-bifu. Unaweza kunyunyiza dawa ya kuzuia kutu baada ya wiki tatu.  
Maharagwe machanga huchukua wiki 9-10 tangu kupanda hadi kuvuna. Hii inategemeana na hali ya hewa pamoja na mbegu.   Maharagwe haya huchanua baada ya wiki sita. Wakati  huu mkulima anatakiwa kuwa makini sana kutokana na uwezekano wa kuwepo wadudu waharibifu kama vile thiripi. Inapende-kezwa kuwasiliana kwa karibu na mta-alamu wa kilimo ili kufanya ukaguzi ili kubaini aina ya wadudu na hatua za kuchukua.


Uvunaji:

 Maharagwe machanga yanafaa kuvunwa viriba vinapokuwa na urefu wa sentimita 11.5-15, unene wa mil-imita 6-8. Hii hufanyika katika wiki ya 9-10. 

Kwa kuanzia, hapo juu ni maelezo mafupi juu ya kilimo hiki.



thanks: ujasiliamali forum group

3 comments:

  1. Asante mkuu,mawasiliano yako yanaweza patikana,ili utoe msaada zaidi?,shukrani za dhati

    ReplyDelete
  2. Asante mkuu,mawasiliano yako yanaweza patikana,ili utoe msaada zaidi?,shukrani za dhati

    ReplyDelete
  3. Hakuna mbegu inayoweza kutoa mavuno mengi na isiyo athiriwa kutokana na hali ya hewa maana naona umependekeza kilimo hiki kinafaa sana ukanda wa barisi

    ReplyDelete